Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Advertise on podcast: Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Rating
5
from
5 reviews
Categories
This podcast has
101 episodes
Language
Publisher
Explicit
No
Date created
2009/03/06
Average duration
6 min.
Release period
1 days

Description

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Podcast episodes

Check latest episodes from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu podcast


UNEA6 ni mwongozo wa kushirikisha pande zote katika kulinda mazingira: Irene Mwoga
2024/02/26
Mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 leo umefungua pazia katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Nairobi, nchini Kenya.  Mkutano huo utakaodumu kwa siku tano unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6000 ikiwa ni pamoja na viongozi wa Mazingira duniani, asasi za kiraia, wataalamu wa Mazingira, maofisa waserikali za mitaa, wakulima, vyama vinavyowakilisha wafanyakazi, jamii zilizoachwa nyuma pamoja na maofisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa. Irene Mwoga mtaalamu wa takwimu wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP kwa bara la Afrika ni Mratibu wa Mkutano huo amezungumza na Stella Vuzo wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Naironi Kenya UNIS na kuhusu mkutano huo dhamira ya mkutano huu unaofanyika kila baada ya miaka miwili, katika mwezi wa Februari akianza kwa kueleza UNEA6 ni nini..
more
26 FEBRUARI 2024
2024/02/26
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 jijini Nairobi, na mradi wa kusaidia watoto na vijana ambao walikuwa na changamoto ya masikio na kuongea nchini Rwanda. Makala tunasalia nchin Kenya na mashinani ukanda wa Gaza, kuikoni? Mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 leo umefungua pazia katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Nairobi, nchini Kenya. Mkutano huo utakaodumu kwa siku tano unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6000 ikiwa ni pamoja na viongozi wa Mazingira duniani, asasi za kiraia, wataalamu wa Mazingira, maofisa waserikali za mitaa, wakulima, vyama vinavyowakilisha wafanyakazi, jamii zilizoachwa nyuma pamoja na maofisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa.Kupitia mradi wa "Winsiga Ndumva", maneno ya lugha ya Kinyarwanda yanayomaanisha "Usiniache nyuma, ninaweza kusikia”, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau wake ikiwemo Wizara ya Afya nchini Rwanda limebadilisha maisha ya watoto wengi na vijana ambao walikuwa na changamoto ya masikio na kuongea kwakuwapatia vifaa maalumu vya kupachika masikioni ili kusaidia masikio kufanya kazi yake ipasavyo. Makala inatupeleka kaunti ya Samburu nchini kenya kuona namna ngamia wanavyoboresha maisha ya wanawake na jamii kwa ujumla.Na mashinani inatupeleka katika ukanda wa Gaza ambapo ongezeko kubwa la utapiamlo miongoni mwa watoto na wanawake wajawazito na wanaonyonyesha ni tishio kubwa kwa afya zao. Shirika la Mpango wa chakula Duniani, WFP linahaha kuwasambazia lishe yenye virutubisho.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
more
UNICEF Rwanda: Programu ya “Winsiga Ndumva” waleta zawadi ya sauti kwa watoto viziwi
2024/02/26
Kupitia mradi wa "Winsiga Ndumva", maneno ya lugha ya Kinyarwanda yanayomaanisha "Usiniache nyuma, ninaweza kusikia”, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau wake ikiwemo Wizara ya Afya nchini Rwanda limebadilisha maisha ya watoto wengi na vijana ambao walikuwa na changamoto ya masikio na kuongea kwakuwapatia vifaa maalumu vya kupachika masikioni ili kusaidia masikio kufanya kazi yake ipasavyo.  Huyo ni Vuguzima Francine, ambaye awali hakujua kuwa mtoto wake kwa kiasi kikubwa ni kiziwi. Mama huyu anasema, “nilikuwa ninamuadhibu kila siku kwa sababu nilikuwa nikimuita haitiki. Nikimwambia aende mahali haiendi. Nilifikiri ni kiburi. Kumbe baadaye ikagundulika hasikii.” UNICEF, kwa zaidi ya watoto na vijana wadogo zaidi ya 500 katika maeneo kadha ya nchini Rwanda imefanya jambo ambalo wazazi na watoto wenyewe wanaona kama miujiza. Manirakora Emmnuel mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika kituo cha viziwi cha Butare akiwa na sura ya furaha na tabasamu pana anasimulia maisha yalivyokuwa magumu kabla hajapata machine ya kusaidia usikivu. “Nilipokuwa ninacheza mpira na watoto wenzangu, mtu akiniambia nielekeze mpira kwake, nilikuwa sisikii. Kwa hiyo kwa kutojua nilikuwa napiga mpira popote.”  Pongezi pia ziende kwa Kitengo cha Manunuzi au Ugavi cha UNICEF kilitekeleza jukumu muhimu kuhakikisha wanavipata visaidizi hivi vya masikio kwa dola 118 kila kimoja ingawa bei yake kwa kawaida inafikia dola 2000 za kimarekani. 
more
Wanawake ili tufanikiwe lazima tujitume: Dkt. Elizabeth Kimani
2024/02/23
Mkutano wa wanawake katika nyanja ya diplomasia umefanyika wiki hii katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya. Viongozi wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi na Geneva Uswisi wamewasilisha mada mbele ya umati wa watu waliohudhuria mkutano huo wakiwemo Mabalozi wastaafu na wanaotumikia nchi zao hivi sasa nchini Kenya kuhusu nafasi ya Mwanamke katika ddiplomasia na katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Dkt. Elizabeth Kimani Murage anayefanyakazi na kituo cha utafiti na idadi ya watu Afrika (African population and research center) kama mtafiri mkuu ni miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo na amezungumza na Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS katika makala hii na anaanza kwa kumueleza kwanini aliona ni muhimu kuhudhuria mkutano huo.
more
Ahunna Eziakonwa: Nimekuja kuona UNDP inavyoweza kuunga mkono maendeleo ya Burundi
2024/02/23
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Kanda ya Afrika, Ahunna Eziakonwa yuko ziarani nchini Burundi ambako amekutana na makundi mbalimbali ya kijamii na hata kufika mpaka wa Burundi na DRC kuona uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo. Pia Bi. Eziakonwa amekutana na Rais Evariste Ndaishimye. “Kwanza kabisa nimemshukuru Rais na nchi kwa kunikaribisha vema katika ziara yangu hii ya kwanza nchini Burundi. Rais na mimi tumejadili mchango wa UNDP katika kuunga mkono maono aliyonayo kwa ajili ya nchi hii. Tunaelewa kwamba kuna maono ya nchi kuwa imechomoza kufikia mwaka 2040 na kuwa imeendelea kufikia 2060. Kama mnavyofahamu UNDP ni shirika la maendeleo na tunataka kuona kile tunachoweza kufanya kuuunga mkono maono haya. Na nimekuja hapa pia kutathimini uimara wa UNDP katika kuisaidia Burundi kwenda katika mwelekeo huu wa maendeleo.” Bi. Eziakonwa anaendelea kueleza waliyoyazungumza na Rais Ndaishimiye akisema, “Pia tumejadili kuhusu vijana. Na nimempongeza Rais kama kinara wa mkutano wa vijana wa Afrika kwa ajili ya amani na usalama ambao ulisababisha kupitisha uamuzi wa Muungano wa Afrika kuhusu mchango wa vijana katika kukuza amani na usalama. Tumezungumza kuhusu vijana kwa ujumla na jinsi ya kuwapa fursa vijana kutumia uwezo wao.” Ni Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Kanda ya Afrika, Ahunna Eziakonwa akiwa ziarani nchini Burundi. Shukrani kwa washirika wetu Mashariki TV ya mjini Bujumbura kwa kufanikisha kutufikishia sauti hii. 
more
23 FEBRUARI 2024
2024/02/23
Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini DR Congo na hali ya msaada wa kibinadamu kwa wakimbizi wake. Pia tunakupeleka nchini Burundi kufuatilia kazi za makundi ya kijamii. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Ukraine tukielekea miaka mwili kamili ya vita nchini humo. Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula duniani WFP leo yametoa wito wa kuchukuliwa hatua mara moja kuwalinda watoto na familia zao waliojikuta katikati ya machafuko yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, huku lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR likielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mustakabali wa zaidi ya raia milioni 7 waliotawanywa na kuomba msaada zaidi kutoka jumuiya ya kimataifa.Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Kanda ya Afrika, Ahunna Eziakonwa yuko ziarani nchini Burundi ambako amekutana na makundi mbalimbali ya kijamii na hata kufika mpaka wa Burundi na DRC kuona uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo. Makala inatupeleka katika chuo kikuu cha Nairobi Kenya ulikomalizika mkutano wa wanawake katika nyanja ya diplomasia. Huko viongozi wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi na Geneva Uswisi wamewasilisha mada mbele ya umati wa watu wakiwemo Mabalozi wastaafu na wa sasa wanaowakilisha mataifa yao Kenya kuhusu nafasi ya mwanamke katika diplomasia na kutimiza malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Dkt. Elizabeth Kimani Murage anayefanyakazi na kituo cha utafiti na idadi ya watu Afrika kama mtafiti mkuu, ni miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo.Katika mashinani tukielekea miaka mwili kamili ya vita nchini Ukraine tutamsikia mmoja wa waathirika wa vita hiyo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
more
Hali DRC si hali tena, mashirika ya UN yataka msaada zaidi na ulinzi kwa raia
2024/02/23
Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula duniani WFP leo yametoa wito wa kuchukuliwa hatua mara moja kuwalinda watoto na familia zao waliojikuta katikati ya machafuko yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, huku lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR likielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mustakbali wa zaidi ya raia milioni 7 waliotawanywa na kuomba msaada zaidi kutoka jumuiya ya kimataifa. Kwamujibu wa WFP na UNICEF idadi kuwa ya watu wakiwemo watoto wamejeruhiwa au kuawa karibu na makazi ya kambi za wakimbizi na yametoa wito kwa pande zote katika mzozo kuwalinda raia na kuruhusu mashirika ya misaada ya kibinadamu  kufanya kazi yao. Mashirika hayo yamesema mapigano ya sasa yamesababisha janga kubwa la kibinadamu na katika wiki mbili zilizopita yamesogea kilometa 25 mwagharibi mwa mji wa Goma kuelekea Sake ambako watoto na familia zao sasa wamezingirwa na mapigano. Mwakilishi wa UNICEF nchini DRC Grant Leaity amesema "Watoto nchini DRC wanahitaji amani sasa. Tunatoa wito kwa watoto kulindwa katika vita hivi na kukomesha ukatili huu kupitia juhudi mpya za kutafuta suluhu za kidiplomasia. Tuna wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa watoto na familia zao walio ndani na karibu na kambi za Goma.” Nalo shirika la UNHCR limesema  mapigano haya yamesababisha msongamano mkubwa wa watu kwenye kambi za wakimbizi ambazo tayari zimejaa pomoni watu waliofurushwa makwao.  Watu zaidi ya 214,000 wamejiunga na watu wengine 500,000 ambao tayari walikimbia hadi maeneo ya karibu na Goma. Shirika hilo limesema linatiwa hofu kubwa kwani hadi sasa zaidi ya watu milioni 7 wametawanywa nchini DRC ukijumuisha na wengine nusu milioni ambao ni wakimbizi na wengi wanakabiliwa na changamoto za hali duni ya malazi, huduma mbovu za usafi na fursa finyu za kujipatia kipato. Ili kushughulikia changamoto hizo na nyingine nyingi za kibinadamu mwaka huu 2024 ombi la dola bilioni 2.6 lilizinduliwa wiki hii kusaidia watu milioni 8.7 wanaohitaji msaada wa kibinadamu DRC. Lakini jana pia UNHCR na washirika wake walizindua mkakati wa kikanda wa ulinzi na msaada kwa DRC unaohitaji dola milioni 668 kusaidia karibu wakimbizi milioni 1 na jamii zinazowahifadhi hasa nchini Angola, Burundi, Jamhuri ya Congo, Rwanda, Uganda, Tanzania na Zambia.
more
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa neno NDONGOSA
2024/02/22
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili  leo ukumbi ni wake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “NDONGOSA.”
more
22 FEBRUARI 2024
2024/02/22
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ambapo FAO limeutenga mwaka huu wa 2024 kuwa wa wanyama wa jamii ya ngamia kwani mchango na faida zake zinanufaisha zaidi ya mataifa 90 duniani na tunaelekea nchini Kenya kwa makala inayohusu ngamia. Pia tunaangazia DR Congo, Gaza na Ukraine kwa muhtasari ya habari. Katika kujifunza kiswahili tunakuletea uchambuzi wa neno “NDONGOSA”. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na wadau wake 105 hii leo wamezindua mpango wa kuwasaidia wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo, DRC pamoja na jamii zilizowakaribisha. Mpango huo uliozinduliwa hii leo jijini Pretoria, Afrika Kusini utakaogharimu jumla ya dola milioni 668 kwa kipindi cha mwaka 2024-2025 unahusisha wadau kutoka Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Angola, Zambia na DRC yenyewe.Kamishna mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA Philippe Lazzarini na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani Dkt. Tedros Ghebreyesus wakiunga mkono tamko la Kamati ya kudumu ya mashirika ya kimataifa (IASC) lililotolewa jana kuhimiza kusitiza mapigano Gaza, kupitia kurasa zao za mtandao wa X wameeleza hali ilivyo tete Gaza. Lazzarini akihoji ni “mara ngapi zaidi tunapaswa kukumbusha kwamba hakuna mahali salama katika Gaza?”  huku Dkt. Tedros akieleza kuwa hospitali zimegeuka uwanja wa vita. Na Uvamizi kamili wa Ukraine uliofanywa na Urusi ukielekea kuingia mwaka wa tatu, Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ametoa wito kwa Urusi kuruhusu Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu na mashirika mengine huru ya kimataifa kuwafikia kikamilifu wale wote ambao wamenyimwa uhuru wao katika muktadha wa vita ya kijeshi. Wakati huo huo nalo Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limeeleza kuwa asilimia 40 ya idadi ya watu wote wa Ukraine bado wanahitaji aina fulani ya usaidizi wa kibinadamu, wakati wakimbizi milioni 2.2 wanahitaji msaada katika nchi za jirani.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “NDONGOSA”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
more
Huku wanakimbia vita wanawake wa Gaza inakuwaje wakiwa katika hedhi?
2024/02/21
Kunapozuka mizozo na machafuko wananchi wote wanaathirika kwasababu maisha yao yanaparanganyika kabisa tofauti na walivyokuwa wamezoea. Watoto waliokuwa wakienda shule sasa hawaendi, si wafanyabiashara, wakulima wala viongozi wa dini wanaotekeleza majukumu yao ya kila siku na suala moja lililo kweli kwa kila mtu ni kuwa wanatafuta kila namna ya kuokoa maisha yao na wengi njia hiyo huwa ni kukusanya virango vyao kidogo wanavyoweza kubeba na kukimbia kuokoa nafsi zao.  Kwa wananchi wa Gaza hususan wanawake wa Gaza, mwezi Oktoba mwaka 2023 mpaka leo wamekuwa wakikimbia mara kusini, mara kaskazini na sasa wapo Rafah karibu na mpaka wa nchi yao na Misri huku wengine wakiwa wamekwama maeneo mbalimbali ya ukanda huo kutokana na mapigano yanayoendelea baina ya wanamgambo wa kipalestina wa Hamas na jeshi la Israel IDF. Lakini ki baiolojia kila mwezi wanawake na wasichana waliovunja ungo huona siku zao au huingia katika hedhi , je wanawezaje kujihifadhi wakati huo huo wakiwa leo hapa kesho pale kuokoa nafsi zao? Tuungane na Leah Mushi katika Makala hii. 
more
21 FEBRUARI 2024
2024/02/21
Hii leo jaridani tunaangazia mizozo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na mabomu ya kutegwa ardhini nchini Ukraine. Makala tukupeleka katika ukanda wa Gaza na mashinani nchini Tanzania, kulikoni? Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Bintou Keita, ameliambia Baraza la Usalama kwamba ana wasiwasi mkubwa kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa unaofanywa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, ambapo vuguvugu hilo linalenga watendaji wa mashirika ya kiraia, hasa watetezi wa haki za binadamu na waandishi wa habari.Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. Makala tunaelekea Gaza ambapo tangu Oktoba 7 mwaka jana kulipozuka machafuko huko Ukanda wa Gaza, wanawake wanaume na watoto wamekuwa wakikimbia kutoka eneo moja Kwenda jingina mpaka sasa wengi wao wapo Rafah karibu kabisa na mpaka wan chi ya Misri lakini umeshajiuliza kwa miezi mitano wanawake wa Gaza wanafanyaje wanapoingia katika kipindi cha hedhi kila mwezi?Mashinani ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya lugha ya mama tutaelekea mjini Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania kumsikia kijana anayetumia Kiswahili kama lugha mama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
more
Paul Heslop: Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa
2024/02/21
Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016.  Paul Heslop Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa utekelezaji wa program ya hatua ya uteguaji mabomu ya kutegwa ardhini ya shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP nchini Ukraine akisema amekuwa akifanya kazi ya uteguzi wa mabomu ya kutegwa ardhini kwa miaka thelathini katika maeneo hatari yenye vita, kuanzia Msumbiji hadi Afghanistan. Lakini aliyoyashuhudia ilikuwa maandalizi tu mtihani kamili ambao sasa uko Ukraine “Ni mazingira magumu sana iwe ya kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiufundi, kwanza kabisa kwa maana ya kieneo, ni nchi kubwa. Kuna mstari wa mbele wa vita ambao sasa ni zaidi ya kilomita elfu moja, kuna uwezekano wa kazi kubwa ya kufanya. theluthi moja ya nchi inashukiwa kuathirika na mabomu ya ardhini. Hiyo ni ukubwa wa kama nchi mbili za Ufaransa.” Mathalani Paul anasema, “Endapo makombora 30,000 yanarushwa kwa siku, hayo ni mabomu 3,000 yasiyolipuka kwa siku. Na, wakati mzozo unafikia siku elfu moja basi, hayo ni mabomu milioni 3 na vilipuzi vingine ambayo hviajalipuka.” Licha a hali kuonekana ni ya kutisha lakini haimkatishi tamaa  Paul wala kumfanya ajutie kufanyakazi ya ya Umoja wa Mataifa ya uteguzi mabomu  “Nimebaini kwamba kufanya kazi kya kutegua mabomu kuwa ni kazi bora zaidi ambayo ningeweza kuwa nayo. Nimeona ushujaa ambao siwezi hata kuamini na nimeshuhudia matukio ambayo yananitia hofu kubwa.” Kwa mujibu wa UNDP ambayo ni mratibu wa hatua za kutegua mabomu ya ardhini Ukraine hadi kufikia Juni mwaka huu mabomu na vilipuzi 540,000 ambavyo havikulipuka vimeteguliwa, lakini kuifanya Ukraine kuwa salama kabisa ni kibarua kigumu na cha gharama kubwa, huku Benk ya dunia ikikadiria kuwa kutegua vilipuzi na mabomu yote nchini humo kutagharimu dola  zaidi ya bilioni 37.
more

Podcast reviews

Read Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu podcast reviews


5 out of 5
5 reviews

Podcast sponsorship advertising

Start advertising on Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu & sponsor relevant audience podcasts


What do you want to promote?

Ad Format

Campaign Budget

Business Details